Mkuu wa mkoa wa Manyara Bwana Erasto Mbwilo katika hali ya utani amesema,mkoa wake unamaambukizi ya kiwango cha chini ya virusi vya Ukimwi ikilinganishwa na Arusha hivyo watu kutoka Arusha wasiingie mkoani mwake.
Mkuu huyo wa Mkoa (pichani)amesema hayo na kutania tena kwamba,anaogopa mabomu baada ya kukaribishwa kuingia mkoani Arusha akipata nafasi.
Utani huo ulijitokeza hivi karibuni wakati Bwana Mbwilo alipokuwa akiukabidhi mwenge wa uhuru kwa mkuu wa mkoa wa Arusha Bwana Magesa Mulongo,ambaye naye alijibu mapigo kwa kuwaambia watu wa manyara kutokuja arusha kwani maambukizi ya ukimwi kwa kiwango cha kitaifa Arusha iko chini kulinganisha na Manyara.
No comments:
Post a Comment